MAGAZETI ya Leo Jumatano 09 July 2025

MAGAZETI ya Leo Jumatano 09 July 2025
MAGAZETI ya Leo Jumatano 09 July 2025
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan atazindua Dira ya Taifa ya 2050 Alhamisi hii ya tarehe 17 Julai 2025, katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo amesema hayo Jumanne ya Julai 8, 2025 katika mkutano wake na wahariri jijini Dar es Salaam.
Profesa Kitila amesema kuwa maandalizi yote ya dira hiyo yamekamilika ikiwemo kupitishwa na Baraza la Mawaziri kisha Bunge kuipokea na kuiidhinisha: “Na hii imepatiwa ulinzi tofauti na iliyopita iliishia Baraza la Mawaziri.”
Amesema kuwa wananchi wa makundi mbalimbali wameshirikishwa ili kupata maoni ya Watanzania. Viongozi tofautitofauti zaidi ya 44 wamehojiwa ili kupata maoni yao.
Profesa Kitila amesema kuwa: “Dira hii 2050 ya Tanzania tuitakayo angalau itatekelezwa na marais si chini ya watatu…”
JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
