MAGAZETI ya Leo Jumamosi 12 July 2025

MAGAZETI ya Leo Jumamosi 12 July 2025
MAGAZETI ya Leo Jumamosi 12 July 2025


Rais wa heshima na mwekezaji wa Simba SC Mohamed Dewji, amevunja ukimya wa muda mrefu na kuweka hadharani mipango ya kuelekea msimu ujao wa mashindano.
Mo Dewji ametumia kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii kuwafikishia ujumbe mashabiki na wanachama wa Simba, ambao wamekosa furaha ya ubingwa kwa misimu minne mfululizo.
Mo Dewji ameandika: Wapenzi wa Simba,
Najua mioyo yenu imebeba maswali mengi. Kama Rais wenu, msione nimekaa kimya wakati tumepitia kipindi hiki kigumu. Kupambania Simba ni wajibu wangu.
Huu siyo wakati wa lawama — ni wakati wa kusimama imara, kuwa kitu kimoja, na kuchukua hatua sahihi za kuleta mabadiliko chanya.
Katika siku chache zijazo, nitazungumza na nyie moja kwa moja. Kuna kazi kubwa inaendelea, na kuna matumaini ya kweli.
Simba haijapotea. Tumekuwa kwenye kipindi cha mpito tumejenga kikosi kipya, tumeimarisha benchi la ufundi, na tumeweka msingi wa mwelekeo mpya. Msimu huu tumefika mbali zaidi ya matarajio, na msimu ujao tunarudi kwa nguvu mpya.
Naomba tuendelee kuwa wavumilivu. Tunahitaji kufanya marekebisho makubwa. Tuendelee kusimama pamoja kama familia moja.
Mbele yetu kuna mwanga. Na kwa pamoja, tutarudi tukiwa imara zaidi, wenye njaa zaidi, na wa kishujaa zaidi.
Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
