MAGAZETI ya Leo Jumamosi 30 August 2025

MAGAZETI ya Leo Jumamosi 30 August 2025
MAGAZETI ya Leo Jumamosi 30 August 2025
Ratiba ya msimu mpya wa Ligi Kuu Soka Tanzania Bara 2025/2026 imetangazwa rasmi, ambapo mashabiki wa soka nchini Tanzania wanatarajia burudani ya hali ya juu kuanzia Septemba 17, 2025.
Taarifa hii ambayo imetolewa August 29, na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), katika raundi ya kwanza, KMC FC watafungua pazia kwa kuvaana na Dodoma Jiji kwenye Uwanja wa KMC Complex jijini Dar es salaam, huku Coastal Union wakiikaribisha Tanzania Prisons Mkwakwani Jijini Tanga.
Mchezo kati ya Young Africans SC dhidi ya Mtibwa Sugar, pamoja na ule wa Simba SC dhidi ya Singida Black Stars, utachezwa baadaye tarehe 29 na 30 Oktoba kutokana na kuwa Katika Michuano ya CAF.
Aidha Ratiba hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia michuano ya kimataifa, kalenda ya FIFA na Mashindano ya Kombe la Shirikisho
Mchezo wa Ufunguzi wa Ngao ya Jamii utachezwa Septemba 16, kati ya Yanga SC dhidi Simba SC katika Uwanja wa Benjamini Mkapa, jijini Dar es salaam.
JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
