TAARIFA Mpya Kwa Waombaji Mikopo HESLB 2025/2026

Filed in Elimu by on 31.08.2025 2 Comments
Share This Post
TAARIFA Mpya Kwa Waombaji Mikopo HESLB 2025/2026

TAARIFA Mpya Kwa Waombaji Mikopo HESLB 2025/2026

TAARIFA Mpya Kwa Waombaji Mikopo HESLB 2025/2026

MATANGAZO YA KAZI BOFYA HAPA

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inapenda kuwafahamisha Waombaji wa Mikopo na Umma kwa ujumla kuwa tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi ya mikopo imesogezwa mbele kutoka tarehe 31 Agosti hadi tarehe 14 Septemba, 2025.

Hatua hii imechukuliwa ili kuwapa fursa wale ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kuwasilisha maombi ya mikopo katika muda uliokuwa umepangwa.

Hadi kufikia tarehe 31 Agosti, 2025, jumla ya maombi ya mikopo 157,309 yameshapokelewa kwa mwaka wa masomo 2025/2026.

Idadi hiyo ni ongezeko la 5% ikilinganishwa na maombi 150,530 yaliyokuwa yamepokelewa katika kipindi kama hiki mwaka jana, 2024/2025.

Aidha, maombi 960 ya ‘Samia Scholarship’ yameshapokelewa ikilinganishwa na maombi 742 yaliyokuwa yamepokelewa mwaka 2024/2025, ikiwa ni ongezeko la 29%.

Itakumbukwa kuwa, Bodi ilianza kupokea maombi ya mikopo ya wanafunzi kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 15 Juni, 2025.

Kupitia tangazo hili, waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2025/2026 ambao wamejisajili lakini hawajakamilisha, wanashauriwa kukamilisha na kuwasilisha maombi yao ya mikopo ndani ya muda ulioongezwa.

Bodi hiyo inapenda kusisitiza kuwa hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza baada ya tarehe 14 Septemba, 2025.

KUTUMA MAOMBI BOFYA HAPA

JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?
Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.

JIUNGE NA GROUP LETU HAPA, GROUP NO 2 HAPA, JIUNGE NA CHANNEL YETU HAPA, JIUNGE NA TELEGRAM HAPA, GROUP NO 3 HAPA, GROUP NO 4 HAPA


Share This Post

Tags:

Comments (2)

Trackback URL | Comments RSS Feed

  1. NGUSA JOHN JOSEPH says:

    HESHIMA ! KWA MAJINA NGUSA JOHN JOSEPH
    UJUMBE : TUNASHUKURURU SANA KWA NIABAA YA WALE WOTE AMBAO TUNATUMA MAOMBI KWA MWAKA HUU TULIOKWISHA KUTUMA NA AMBAO WANAENDELEA KUTUMA
    KWA KUTUPA NAFASI HII YA KUONGEZEWA MUDA IKIONESHA DHAHILI HALI YA KUTHAMIN NA KUTUJALI
    IKAWE KHERI KATIKA MAJUKUMU YENU MUNGU AWATIE WEPESI NA JUHUDI KATIKA KULIJENGA TAIFA
    AHSANTENI SANA

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *