MAGAZETI ya Leo Jumanne tarehe 16 September 2025

MAGAZETI ya Leo Jumanne tarehe 16 September 2025
MAGAZETI ya Leo Jumanne tarehe 16 September 2025
Klabu ya Singida Black Stars imetwaa ubingwa wa Kombe la Kagame 2025 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Al Hilal ya Sudan, Septemba 15, 2025 katika Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.
Nyota wa Singida Black Stars, alikuwa kiungo Mzambia Clatous Chama ambaye ndiye alipachika mabao yote mawili yaliyoipa ushindi timu yake.
Bao la kwanza alifunga katika dakika ya 20 ya mchezo lakini lilidumu kwa dakika 11 tu kwani Al Hilal ilisawazisha katika dakika ya 31 kupitia kwa Taha Abdelrazig na hadi filimbi ya mapumziko ilipopulizwa timu hizo zilienda katik vyumba vya kubadilishia nguo zikiwa sare ya bao 1-1.
Ushindi huo umeifanya Singida Black Stars kutwaa kwa mara ya kwanza taji la mashindano hayo ikifuata nyayo za timu nyingine za Tanzania, Simba, Yanga na Azam ambazo zimewahi kuchukua Kombe hilo.
Baada ya mchezo, Clatous Chama ameibuka mshindi wa Tuzo za Mchezaji Bora wa Mechi na Mfungaji Bora wa Mashindano huku Metacha Mnata akishinda tuzo ya Kipa Bora.
JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
