NAFASI Za Kazi Busokelo District Council

NAFASI Za Kazi Busokelo District Council
NAFASI Za Kazi Busokelo District Council
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo anatangaza nafasi 20 za mgambo wa mapato kwaajili ya kukusanya mapato ndani ya Halmashauri.
SIFA ZA MWOMBAJI:
- Awe raia wa Tanzania.
- Awe na umri wa kuanzia miaka 25 hadi 45.
- Awe na Elimu kuanzia kidato cha nne.
- Aliyepata mafunzo ya Mgambo au JKT-atapewa kipaumbele.
- Asiwe na historia ya kosa lolote la jinai.
- Awe tayari kupangiwa kituo chochote cha kazi ndani ya Halmashauri.
KAZI NA MAJUKUMU:
- Kukusanya mapato ya Halmashauri kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato vilivyopo katika eneo la Hamashauri ya Wilaya ya Busokelo kwa kutumia mashine ya kieletroniki(POS).
- Kuwasilisha benki kupitia akaunti ya mapato ya Halmshauri makusanyo yote yaliokusanywa ndani ya saa 24 katika siku za kazi au siku ya kwanza ya kazi ya wiki au baada ya sikukuu.
- Kutoa risiti za mashine ya kielektoniki (POS) kiasi sawa na fedha atakayolipa mlipaji.
- Kutunza vifaa vya kukusanyia mapato (POS) rejista ya nyaraka za benki au Halmashauri zinazothibitisha uingizaji wa fedha benki.
- Kufanya uhakiki kila siku wa makusanyo ya siku na taarifa ya mashine ya kukusanyia mapato.
- Kuwasilisha Halmashauri mashine ya kukusanya mapato kwa ajili ya ukaguzi/Uchunguzi kila inapohitajika.
- Kufanya kazi zingine zinazohusu mapato kadri utakavyoelezwa na mwajiri.
- Kutunza kumbukumbu za takwimu za mapato katika vitabu mbalimbali getini.
- Kukagua nyaraka na ulipwaji ushuru katika magari ya mizigo,magari ya abiria na chombo chochote cha usafiri kilichobeba mizigo
- Kufanya ukaguzi muda wote (masaa 24) ya siku.
MASHARTI YA JUMLA KWA MUOMBAJI.
- Siku ya usaili kila muombaji afike na vyeti halisi (Original) vya Elimu, kuzaliwa na Kitambulisho.
- Uwasilishwaji wa taarifa na sifa za kughushi ni kosa kisheria na wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.
- Maombi yaambatishwe na nakala ya kitambulisho cha NIDA.
Maombi yote yapelekwe kwa mkono ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Busokelo.
Mwisho wa Kutuma Maombi ni tarehe 29/09/2025 saa 9:30 Alasiri.
JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
