VYUO Kufunguliwa 17 November 2025

VYUO Kufunguliwa 17 November 2025
VYUO Kufunguliwa 17 November 2025
Baada ya kusogezwa mbele kwa ratiba ya kufungua taasisi za elimu ya juu kufuatia vurugu zilizotokea Oktoba 29, Serikali hatimaye imetangaza tarehe mpya ya kurejea vyuoni kwa wanafunzi.
Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia iliyotolewa leo Novemba 8, 2025, vyuo vyote vya umma na binafsi vitafunguliwa kuanzia Novemba 17.
Awali, wanafunzi wa mwaka wa kwanza walipaswa kuripoti Novemba 1 na wanaoendelea Novemba 3, lakini ratiba hiyo iliahirishwa kwa sababu za kiusalama kufuatia maandamano yaliyosababisha vurugu zilizosababisha vifo na uharibifu wa mali na miundombinu.
Kwa ratiba mpya, wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanatakiwa kufika kuanzia Novemba 17 kwaajili ya programu maalumu ya utangulizi, huku wanafunzi wanaoendelea wakitarajiwa kurejea rasmi kuanzia Novemba 24.
Katika taarifa hiyo iliyosainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Carolyne Nombo, Serikali imewataka wanafunzi kufika kwa wakati na kuzingatia ratiba zote za kitaaluma.
JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
