UFADHILI Wa Masomo Nchini Uturuki 2026/2027

UFADHILI Wa Masomo Nchini Uturuki 2026/2027
UFADHILI Wa Masomo Nchini Uturuki 2026/2027
Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uturuki unapenda
kuujulisha umma wa Watanzania kwamba Serikali ya Jamhuri ya Uturuki kupitia mpango wa ufadhili wa masomo (Türkiye Bursları) kwa mwaka 2026/2027, imeongeza muda wa kupokea maombi ya ufadhili wa masomo katika Shahada ya Kwanza, Uzamili na Shahada ya Uzamivu hadi kufikia Februari 25, 2026 (saa 5:59 usiku, majira ya Uturuki).
Ufadhili huo unajumuisha ada ya masomo, posho ya kujikimu, malazi, bima ya afya, tiketi ya ndege kwenda Uturuki na kurudi, udahili wa chuo na usajili wa kozi, utafiti na mafunzo ya Lugha ya Kituruki.
Taarifa zaidi kuhusu ufadhili huo ikiwemo sifa na taratibu za uombaji zinapatikana kupitia tovuti (https://turkiyeburslari.gov.tr).
Maombi kuhusu ufadhili huo yalifunguliwa kuanzia Januari 10, 2026 na mwisho wa kutuma maombi ni Februari 25, 2026.
JE, UNATAFUTA AJIRA LEO?Jiunge na Watanzania Wengine Kupata Matangazo ya Ajira Kila Siku Kutoka Serikalini Pamoja na Makampuni Mbalimbali Leo Gusa HAPA
Share Kwa Ndugu, Jamaa na Marafiki nao wapate Fursa hizi Kila Siku.
