MAGAZETI ya Leo Ijumaa 04 October 2025

MAGAZETI ya Leo Ijumaa 04 October 2025
MAGAZETI ya Leo Ijumaa 04 October 2025
Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA) kupitia Pori la Akiba la Kijereshi, imefanikiwa kuwaua fisi 17 katika Kata ya Shigala, Wilaya ya Busega, mkoani Simiyu, kufuatia operesheni maalumu inayoendelea ya kuwasaka wanyama hao waharibifu.
Operesheni hiyo imechochewa na matukio ya mara kwa mara ya fisi kuvamia makazi ya wananchi na kusababisha madhara makubwa, ikiwemo vifo vya watoto pamoja na kuua mifugo ya wananchi wa eneo hilo.
Hata hivyo, wananchi walieleza kushangazwa na hali ya baadhi ya fisi waliokamatwa katika operesheni hiyo, ambapo baadhi walikutwa wakiwa na shanga shingoni huku wengine wakiwa wameandikwa majina sehemu za paja la miguu.
Mamlaka ya TAWA imeeleza kuwa operesheni hiyo itaendelea ili kuhakikisha usalama wa wakazi wa eneo hilo na mali zao unadumu.
