NAFASI 114 Za Kazi Chemba District Council

NAFASI 114 Za Kazi Chemba District Council
NAFASI 114 Za Kazi Chemba District Council
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA WAKUSANYA MAPATO VIJIJINI – NAFASI 114 REVENUE COLLECTORS
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba anawatangazia Wananchi wote wenye sifa, nafasi 114 kazi ya kukusanya mapato kama ifuatavyo:-
SIFA ZA MUOMBAJI:
- Awe raia wa Tanzania.
- Awe na umri kuanzia miaka 18 na kuendelea.
- Awe na elimu kuanzia Darasa la Saba na kuendelea.
- Awe ni mkazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba.
- Awe na mdhamini atakaye mdhamini wakati wa
kujaza mkataba (mke, mume, baba, mama au mtu yeyote mwenye mali isiyo hamishika kama vile shamba, nyumba n.k). - Awe hajawahi kupatikana na kosa lolote la jinai au kuhukumiwa kifungo jela katika Mahakama yoyote.
- Awe tayari kufanya kazi katika eneo lolote ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Chemba.
- Yeyote aliyewahi kufanya kazi Halmashauri na kuisababishia hasara au upotevu wa mapato au kudaiwa na Halmashauri, HARUHUSIWI KUOMBA KAZI HII.
- Awe na namba ya NIDA itakayo tumika wakati wa usajili wa Mkusanya Mapato.
MASHARTI YA KUOMBA:
- Barua ya maombi ipitie kwa Afisa Mtendaji wa Kijiji au Kata.
- Barua iambatane na picha ya muombaji na mdhamini wake zilizo pigwa siku za karibuni.
MAJUKUMU YA MKUSANYA MAPATO.
- Kukusanya mapato ya Halmashauri kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato vilivyopo katika eneo la Wilaya ya Chemba atakalopangiwa kufanya kazi kwa kutumia mashine ya Kielektroniki (POS).
- Kuwasilisha benki kupitia akaunti ya mapato ya Halmashauri makusanyo yote yaliyokusanywa kwa wakati katika siku za kazi au siku ya kwanza ya kazi ya wiki au baada ya sikukuu.
- Kutoa risiti za Mashine ya Kielektroniki (POS) kiasi sawa na fedha atakayopokea kutoka kwa mlipaji.
- Kutunza vifaa vya kukusanyia mapato (POS, Rejista) na Nyaraka za benki au Halmashauri zinazothibitisha uingizaji wa fedha benki.
- Kufanya uhakiki kila siku wa makusanyo ya siku na taarifa ya mashine ya kukusanyia mapato na kuiwasilisha.
- Kuwasilisha Halmashauri mashine ya kukusanyia mapato (POS) kwaajili ya Ukaguzi /uchunguzi na.
- Kufanya kazi nyingine zinazohusu mapato kwa kadri atakavyoelekezwa na Mwajiri.
MUDA/ MASHARTI YA AJIRA.
- Ajira hii ni ya Mkataba wa miezi sita kuanzia mwezi Agosti 2025 hadi Januari 2026.
- Atakuwa chini ya uangalizi wa Mtendaji wa Kata na Kijiji husika na.
- Mkusanyaji ataongezewa mkataba kutokana na juhudi yake katika ukusanyaji wa mapato.
MALIPO YA MKUSANYA MAPATO
Malipo kwa kazi ya ukusanyaji mapato yatakuwa ni asilimia 5 (5%) ya mapato aliyokusanya na kuyawasilisha Benki kwa wakati
Maombi yatumwe ifikapo au kabla ya tarehe 28 Julai, 2025 kwa:
MKURUGENZI MTENDAJI,
HALMASHAURI YA WILAYA,
S. L. P. 830,
CHEMBA.
Mwisho wa Kituma Maombi ni tarehe 28 Julai 2025 saa 9.30 mchana.
