MAGAZETI ya Leo Jumatatu 23 June 2025

MAGAZETI ya Leo Jumatatu 23 June 2025
MAGAZETI ya Leo Jumatatu 23 June 2025


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amesema Wizara hiyo itaendelea kuwalinda Watanzania kwa kusimamia maudhui mbalimbali mtandaoni ikiwamo mitandao ya kijamii ili kuhakikisha sheria na taratibu za nchi zinafuatwa ambapo amesema mtandao wa X umefungwa Tanzania kwakuwa unaruhusu maudhui ya ngono.
Akiongea June 22,2025 Jijini Dar es salaam kwenye Cafe Talk, Jerry Silaa amesema “Platform ya X ina vitu ambavyo vinaenda kinyume na kanuni, sheria, taratibu, mila na desturi, leo wapo Watoto wana simu kazi yetu ni content kwenye simu ya Mtoto, sio kwa X tu platform yoyote ikienda kinyume tutachukau hatua, X kuna picha za ngono Youtube hauwezi kuzipata, X kuna hadi content za mapenz ya jinsia moja kazi yetu kumlinda mlaji”
