KUITWA Kazini Kusimamia Uchaguzi Mkuu 2025 Tunduma Town Council

KUITWA Kazini Kusimamia Uchaguzi Mkuu 2025 Tunduma Town Council
KUITWA Kazini Kusimamia Uchaguzi Mkuu 2025 Tunduma Town Council
Kwa madhumuni ya Uendeshaji wa Uchaguzi Mkuu na kwa kuzingatia masharti ya kifungu cha 6(5) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na.1 ya Mwaka 2024, kikisomwa pamoja na Kanuni za Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani za Mwaka 2025, pamoja na kuzingatia Ratiba ya utekelezaji wa shughuli za Uchaguzi Mkuu mwaka 2025. Msimamizi wa Jimbo la Tunduma anawatangazia watendaji wa vituo vya Kupiga Kura waliochaguliwa kwa nafasi za Wasimamizi wa vituo, Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo na Makarani Waongozaji wa Vituo vya kupigia Kura kuhudhuria mafunzo ya kazi hiyo.
Mafunzo hayo yatafanyika katika Ukumbi wa Shule ya Msingi Elisabene iliyopo Chapwa kuanzia saa 1:00 asubuhi kwa tarehe zifuatazo:-
- Tarehe 25 Oktoba, 2025 -Makarani Waongozaji wa Vituo vya Kupigia Kura.
- Tarehe 26-27 Oktoba, 2025 Wasimamizi wa Vituo na
Wasimamizi Wasaidizi wa Vituo vya Kupiga Kura
Watendaji wote wanatakiwa kuzingatia yafuatayo:-
- Muda wa mafunzo ni kuanzia saa 1:00 Asubuhi
- Fika ukiwa na kitambulisho chochote kinachokutambulisha
Orodha ya Majina ya Waliochaguliwa Kuhudhuria Mafunzo Imeambatishwa hapa chini kwenye PDF.
DONWLOAD PDF YA MAJINA HAPA
