MAJINA ya Walioitwa Kazini Tanganyika District Council

MAJINA ya Walioitwa Kazini Tanganyika District Council
MAJINA ya Walioitwa Kazini Tanganyika District Council
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika anapenda kuwatangazia waliofanya Usaili tarehe 04-05.06.2025 kwamba waliofaulu usaili wanatakiwa kuripoti kazini siku ya Jumatatu tarehe 30.06.2025.
Walioitwa waripoti kazini katika Makao Makuu ya Halmashauri yaliyopo katika Kijiji cha Majalila Kata ya Tongwe.
Mambo ya kuzingatia: –
- Wanatakiwa kuja na vyeti halisi vya shule na taaluma
- Wanatakiwa kuja na cheti halisi cha kuzaliwa.
- Wanatakiwa kuja na Kitambulisho cha Taifa (NIDA) au namba husika.
- Wanatakiwa kuja na picha mbili za rangi za ukubwa wa “passport”.
Ni muhimu walioitwa wote kufika siku iliyotajwa kwaajili ya Mafunzo (Orientation Course)
Kwa wale ambao majina yao hayamo katika Tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine tena nafasi za kazi zitakapotangazwa kwa kuzingatia sifa zao.
Orodha ya Majina ya Walioitwa Kazini Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika imeambatanishwa hapa chini.

Tags: MAJINA ya Walioitwa Kazini Tanganyika District Council
